MASHIRIKA ya Kiraia ya Afrika (CSOs) yametoa tamko lenye hoja tano kuhusu malengo ya nishati mbadala kwa Afrika katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi(28) unaoendelea Dubai,Falme za Kiarabu.
Moja ya vipaumbele vya Afŕika katika COP28 ilikuwa kupata mikataba ambayo ingewekeza mara tatu katika nishati mbadala katika bara baada ya Mkutano wa Kilele wa Hali ya Hewa wa Afŕika kushindwa kutoa matokeo kabambe kuhusu nishati mbadala.