By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
MESHAMESHAMESHA
  • Home
  • Who We Are
    • About
    • Management
    • Strategic Plan, 2023-2027
  • Sayansi Magazine
  • Media
    • Audio
    • Videos
    • Photos
  • Membership
    • Accredited Members
    • How to Join MESHA
  • IFAJ 2025 Congress
Search
Categories
  • Climate Change
  • Health
  • Biodiversity
  • Agriculture
  • Environment
© 2024 MESHA. All Rights Reserved.
Reading: Teknolojia ya uvunaji wa maji: Kumaliza tatizo la uhaba wa chakula nchini
Share
Sign In
Notification Show More
Font ResizerAa
MESHAMESHA
Font ResizerAa
Search
  • Home
  • Who We Are
    • About
    • Management
    • Strategic Plan, 2023-2027
  • Sayansi Magazine
  • Media
    • Audio
    • Videos
    • Photos
  • Membership
    • Accredited Members
    • How to Join MESHA
  • IFAJ 2025 Congress
Have an existing account? Sign In
Follow US
© 2024 Mesha. All Rights Reserved.
MESHA > Blog > Agriculture > Teknolojia ya uvunaji wa maji: Kumaliza tatizo la uhaba wa chakula nchini
Agriculture

Teknolojia ya uvunaji wa maji: Kumaliza tatizo la uhaba wa chakula nchini

Mesha
Mesha Published 18 April 2023
Share
3 Min Read
SHARE
Daktari Esther Gikonyo/Picha:Robert Malala

By RUTH KEAH

Shirika la kilimo na utafiti la Kenya (KALRO) tawi la Kabete linapatikana takriban kilomita 13 kutoka jijini Nairobi nchini Kenya.

Upande wa kulia mita chache tu baada ya kuingia kwenye lango kuu,unakutana na shamba lenye ukubwa wa ekari moja. Lilikuwa kivutio kikuu kwa watu waliotembelea shirika hilo siku ya maonyesho ya kilimo.

Hii ni kutokana na mazao yaliyonawiri, sio tu kwa rangi yake ya kupendeza ya kibichi, bali pia kwa ubora wa mazao hayo licha ya kuwa ni msimu wa kiangazi.

Shirika hilo,limekuwa likitumia teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua, na kisha kunyunyuzia shamba hilo.

Daktari Esther Gikonyo ni mkurugenzi mkuu wa shirika la KALRO tawi la Kabete,yeye pia ni mtaalamu katika sekta ya rotuba ya udongo.

Alisema teknolojia hiyo ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wakulima wanatumia ili kuvuna chakula cha kutosha.

Daktari Esther Gikonyo alisema,kama shirika, walilima shamba hilo mwezi wa Januari na Februari na kunyunyizia maji mazao hayo kwa kutumia maji ambayo walivuna.

Alisema endapo jamii itakumbatia teknolojia ya uvunaji wa maji, basi kila familia itaweza kujitegemea kwa kupata chakula kila siku.

Zaidi, Daktari Gikonyo aliwashauri wakulima kujenga tabia ya kuvuna maji ya mvua hasa katika kipindi ambacho mvua ni chache na haziendani na kalenda ya wakulima.

Sawia kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamekuwa yakisababisha kukosekana kwa mvua za kutosha na uharibifu wa mazingira.

Hali hiyo imewasababisha wakulima kupata mazao kidogo ama kutovuna kabisa.

Jambo ambalo limekuwa likisababisha baadhi ya maeneo nchini kuwa hatarini kukumbwa na baa la njaa.

 Uvunaji wa maji ya mvua.

Uvunaji wa maji ni mbinu ambayo inazuia maji ya mvua kutiririka hovyo.

Badala yake, maji hukusanywa na kuhifadhiwa na kutumiwa baadaye na watu,wanyama ama kwa kunyunyizia mimea

Francis Karanja ni mhandisi, pia ni mtaalamu anayehusika na teknolojia ya uvunaji wa maji.

Mhandisi Karanja alisema teknolojia hiyo ya uvunaji wa maji ni rahisi na kila mkulima anaweza kuimudu.

“Baadhi ya vifaa ambavyo tulitumia ni karatasi nyeusi ya kufunika bwawa, matangi mawili ya maji ambayo huvutwa kwa kutumia nguvu za miale ya jua.”

Kulingana na mhandisi Karanja, bwawa hilo lina uwezo wa kubeba maji lita 4,500.

Na linaweza kulima shamba la ukubwa wa ekari moja kwa kipindi cha miezi mitatu kukuza aina tofauti tofauti ya mboga.

Mhandisi Karanja alisema bwawa hilo liliwagharimu takriban shilingi laki mbili na elfu hamsini. Huku likitarajiwa kudumu kwa zaidi ya miaka kumi.

Washikadau mbalimbali walionyesha teknolojia mbalimbali wanazotumia kufanya ukulima.

Baadhi yao ni wanafunzi kutoka shule ya msingi ya Kangemi jijini Nairobi.

Wanafunzi walio kwenye kikundi cha kilimo cha 4K Club, wakionyesha weledi wao wa kukuza mazao hasa mboga kupitia teknolojia mbalimbali.

Huku wakitumia maji hayo yaliyovunwa kukuza mboga zao.

Makala haya yamefanikishwa kwa usaidizi kutoka kwa muungano wa wanahabari wanaoandika habari za sayansi(MESHA).

       

You Might Also Like

Andermatt to enlighten IFAJ fete delegates on regenerative farming and biological innovation

Joy in western Kenya as farmers abandon tobacco for beans

Sowing Success: How Ghana’s Local Content Policy Could Revolutionize the Seed Industry

Feared Sweetpotato disease continues to ravage crop’s production: Report

Malawi seed sector amplify support for biotech

Sign Up For Daily Newsletter

Be keep up! Get the latest breaking news delivered straight to your inbox.

By signing up, you agree to our Terms of Use and acknowledge the data practices in our Privacy Policy. You may unsubscribe at any time.
Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp LinkedIn Email Copy Link Print
What do you think?
Love0
Sad0
Happy0
Sleepy0
Angry0
Dead0
Wink0
Previous Article Pastoralists reclaim land from invasive plant that kills other vegetation, grasslands
Next Article Paying tribute to midwives around the world
MESHA gets boost to implement project on Africa-led climate stories
Climate
Presentations from MESHA’s Science Café: Framing Reproductive Health Stories Through Solutions Journalism and Lived Reporting Experiences
Solutions Journalism
Stakeholders out to tackle climate induced malaria surge at Kenya’s coast
Health
Build audience trust through solutions journalism, journalists told
Solutions Journalism

Contact Info

Location
Oasis Apartments, Jogoo Road, 3rd Floor
Phone
+254 721 578517
+254 732 229 230
info@meshascience.org

Facebook

//

We are the number one science, health and agriculture journalists network in Africa accessed by over 20 million users.

Quick Link

  • About
  • Sayansi Magazine
  • Accredited Members
  • Mesha Audio
  • My Bookmarks

Top Categories

  • Climate Change
  • Health
  • Biodiversity
  • Agriculture
  • Environment

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MESHAMESHA
Follow US
© 2024 MESHA. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.
Welcome Back!

Sign in to your account

Username or Email Address
Password

Lost your password?